Saturday, February 16, 2013

TCIB yazindua kituo cha taarifa vijijini

Mwenyekiti wa kijiji cha Miswechini wilayani Kibaha (mwenye kofia) bwana Dunia Mrisho akiwa na mkurugenzi mtendaji wa TCIB bwana Deus Kibamba (katikati) wakimgawia  machapisho mwana kijiji wa Miswe wakati wa ufunguzi wa ofisi ya kituo cha taarifa kijijini hapo juzi. (Picha na Elisha Magolanga)

Na Elisha Magolanga

Kibaha. Jamii kubwa ya watanzania  waishio vijijini wanakabiliwa na tatizo la kukosa taarifa nyingi za kijamii hususani zile zinazohusu maendeleo na maisha yao ya kila siku.

Akizungumza na wanakijiji wa Miswechini kata ya Mbwawa wilayani Kibaha wakati wa uzinduzi wa kituo cha taarifa vijijini, Mkurugeni wa Kituo cha taarifa kwa wananchi (TCIB), bwana Deusi Kibamba alisema kupata taarifa ni haki yakila mtanzania bila kujali mahali anakoishi, umri na jinsia ya mtu.

Bwana Kibamba alisema kuwa kituo kilichofunguliwa kijijini hapo kituo kitatoa fulsa kwa wana kijiji kujipatia taarifa mbalimbali za kijamii, za kisheria na habari kuhusu mambo mbalimbali yanayotokea nchini.

“Wanakijiji katika kituo hiki watapata fursa ya kujisomea majarida, magazeti na tafiti mbalimbali ikiwa ni pamoja na kutazama luninga na kufanya majadiliano ya pamoja hapa kituoni,” alisema Kibamba.

Kwa upande wake mwenyekiti wa kijiji hicho bwana Dunia Mrisho aliwataka wanakijiji wote watumie vizurifursa  iliyotolewa  na TCIB kwa ajiliya kujiongezea maarifa ili waweze kushiriki kikamilifu katika kuchangia maendeleo ya kijiji na taifa kwa kufuatilia kwa ukaribu mambo mbalimbali yanayowahusu.

Akiongelea malengo ya kituo cha taarifa vijijini, mratibu wa mradi huo, Obeid Mkina alisema kuwa upatikanaji wa taarifa sahihi unamfanya  mwananchi kuwa na ufahamu wakutosha juu ya masuala mabalimbali yonayoizunguka jamii yake hivyo hujiamini na kushiriki kikamilifu katika maendeleo ya jamii.

Mkina aliongeza kuwa mradi huo wa taarifa vijijini ni miongoni mwa miradi mingine minne inayodhaminiwa na TCIB katika vijiji vilivyoko Mwanhuzi na Meatu mkoani Simiyu, Kitonga mkoani Iringa na Micheweni visiwani Pemba ambapo kila kituo kimepewa luninga na king’amuzi, magazeti, majarida ya taarifa za afya na machapisho ya katiba.

Wednesday, February 13, 2013

Form six sit for final exams


By Elisha Magolanga

 
Dar es Salaam. About 52,612 Form VI students in the country on Monday started sitting for  their national examinations scheduled to end on February 27,  said the National Examinations Council of Tanzania (NECTA).

NECTA Public Relations Officer, John Nchimbi said that 43, 309 are school candidates while 9203 are private candidates. He noted that among them 37 students with eyes disability are sitting fro exams where 28 are school candidates and 9 are private candidates.
This year the number of candidates sitting for form six exams has dropped down for 2317 candidates behind last year as 54,929 candidates sat for final examinations.

Mr. Nchimbi said that examination excise has started well since there was no any problem reported in the initial exams. He made a call to all education officers to ensure all procedures are followed as he caution to candidates to stay away from malpractice saying legal steps would be taken.  

The Citizen made surveillance in the city’s schools starting at Shaaban Robert, Tambaza, Azania, Jangwani, Zanaki, and Mzizima Secondary schools where students were in good condition doing their examinations under tight security established in each school. 

Shaaban Robert Headmaster, Mr S. Ramji told the reporter that in his school all 66 student sat for their final exams and students were well physically and psychologically. He added that there was no any difficulty there since examinations arrived and stared on time. 

Peter Muhondajile HKL Azania candidate said, “Initial examinations have started well, as in our class no candidate has missed done examinations,” He added that Kiswahili examination was quite fair since it has covered the given syllabuses as teachers have already taught.
In other occasion, schools headmasters’ ad invigilators refused to comment anything arguing that they are not in position to comment as the spokesperson was the District Education Officers. The paper tried to get the officers call but was not responded.  

CSOs: Spekaer seat abuse parliamentary principles


LHRC Executive Director Dr Hellen Kijo Bisimba 
 By Elisha Magolanga

Dar es Salaam. Civil Society Organization's yesterday said that party’s favoritism done by the Speaker seat has dropped moral value of the parliamentary before the community.

Also, the parliament principles number 115 and 116 (8) which are in accordance with the constitution, the Speaker has no power to break some important parliament committees including the Public Organisations Account Committee (POAC).

The statement has come after Legal and Human Rights Centre (LHRC) and The Citizens’ Parliament Watch (CPW) conduct a close follow-up on the 10th on-going parliamentary sessions that was ended last week.

The study conducted by joint organisation has revealed that the Speaker, Deputy Speaker and some of chairpersons of parliamentary sessions have been abusing the seat aggressively resulting in failure to run the parliament in a stable condition.
In contrast, the CSO have congratulated parliament session’s chairperson, Ms Jenista Mhagama that has been improving significant changes in the management of parliamentary sessions following the parliamentary principles mounted without bias.

In the 10th parliament session ended last week, the Opposition geared up to table a no-confidence vote against the Speaker Anne Makinda and her deputy, Job Ndugai, allegedly for favouritism. Allegations came after Ms Makinda and Mr Ndugai recently quashed private motions by Ubungo MP, Mr John Mnyika (Chadema) and nominated MP, Mr James Mbatia. The latter doubles, as chairman of another opposition party, NCCR-Mageuzi. 

MPs from Chadema, NCCR Mageuzi and Tanzania Labour Party said to be “disappointed” by the way the two are handling House affairs and have vowed to invoke parliamentary standing orders to table a motion of no-confidence against the two officials.

Addressing Journalists in Dar es Salaam yesterday, LHRC Executive Director Dr Hellen Kijo Bisimba said that although the 2011 and 2012 CPW report recommended the Speaker seat should manage principles without biases, the organisation has realised there still some weakness that should be addressed, and congratulate Ms Mhagama for her improvement as the report recommended.

On the side of breaking parliamentary committee Dr Bisimba said "POAC has broken at the middle process of Mtwara gas contracts which had begun to be addressed, also it has ordered to prevent social security funds to lend to government without contracts agreement between the bags and the government,”

She added that in the 10th parliament three important motions from opposition parties were burned in unsatisfactory conditions while two from the ruling party were agreed without any opposition. 

“The rejected three motions suggested by opposition were very crucial for Tanzanian future. These include education curriculums, water supply in Dar es Salaam city and the motion on the trends of the National Examinations Council of Tanzania,” she noted.

Furthermore, poor MPs attendance was among the problems that affect decision making in the parliament. Dr. Bisimba added, “In 6th of February 2013, the Bunge failed to provide declaration to join two international contracts because of small number of MPs attended.

“The government has lost Sh 321,300,00 due to useless of 12 hours without parliamentary session while more than 82 government and CSO professionals stayed without job spending government money in Dodoma for clarification on the international contracts,” 

The Organisations has urged MPs to understand that their presence in the parliament is for the public interest and not for their parties. Also, the seat has advised to put priority on motions that touch the human life instead of political fanaticism.  
 













Wednesday, June 13, 2012

Ziara za Pinda zalalamikiwa bungeni

Wananchi wadai kuchangishwa mbuzi kwa mabavu

Na mwandishi wetu

MBUNGE wa Viti Maalumu (Chadema), Rose Kamili ameilalamikia  Ofisi ya Waziri Mkuu, akisema mtendaji mmoja wa Serikali alikamatwa kutokana na kushindwa kukusanya mchango wa mbuzi tisa za zawadi kwa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda wakati wa ziara yake Wilaya ya Maswa, mkoani Simiyu.

Kamili aliyasema hayo, wakati akiuliza swali la nyongeza kwa Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu (Tamisemi), Aggrey Mwanri baada ya swali la msingi lililoulizwa na Mbunge wa Maswa Mashariki, Sylvester Kasulumbayi (Chadema), kuhusu mipaka ya madaraka kati ya Serikali za Mitaa na Serikali Kuu kiutendaji.

Aidha, Kamili aliongeza kusema kuwa Mkuu wa Wilaya ya Maswa aliwaagiza watendaji wote wa kata kukusanya mbuzi ikiwa ni zawadi za ujio wa Waziri Mkuu katika wilaya yao na kwamba walioshindwa walikamatwa.

Akijibu swali hilo, Mwanri alisema ofisi yake haina taarifa ya tuhuma hizo na kumtaka mbunge huyo azithibitishe. Alisema Serikali haina utaratibu wa kuomba kupewa zawadi mbalimbali kwa viongozi wake na kama mbunge huyo ana ushahidi wa suala hilo autoe.

Mara baada ya majibu hayo, Spika wa Bunge, Anne Makinda alimpa fursa mbunge huyo kueleza kama anao ushahidi huo na akajibu kuwa anao kwani aliona hata kupitia luninga Waziri Mkuu Pinda akikabidhiwa zawadi.

Kwa upande mwingine, Kamili aliulizia juu ya operesheni ya kuhamisha wakazi wa pori la Maswa ambao nyumba zao kadhaa zilichomwa moto na wafugaji kadhaa kutimuliwa bila kujua pa kwenda.

Akijibu swali hiyo, Mwanri alisema mgogoro huo wa kuhamishwa wananchi hao, tayari ulifuatiliwa na Serikali na Waziri wa Nchi, Tamisemi wakati huo, George Mkuchika alikwenda katika eneo hilo na kuzungumza na wananchi na kupata taarifa sahihi.

Hata hivyo, alisema wananchi wa vijiji saba vya eneo hilo, walikubaliana kuanzisha Hifadhi ya Jamii (WMA) na kutoa eneo hilo kwa mwekezaji jambo ambalo lilitekelezwa.

Awali, akijibu swali la Kasulumbayi, Naibu Waziri Mwanry alisema wakuu wa mikoa na wilaya nchini, hawaruhusiwi kwa mujibu wa sheria, kuingilia utendaji kazi wa mamlaka za Serikali za Mitaa, ikiwa zinatekeleza majukumu yake kwa kuzingatia sera, sheria, kanuni na miongozo iliyowekwa na Serikali.


Kasulumbayi alitaka kujua inakuwaje wakuu wa mikoa na wilaya ambao kiutendaji ni watumishi wa Serikali Kuu, wanatoa amri kwa watendaji walio chini ya wakurugenzi wa wilaya, kuhamisha wananchi katika maeneo yao. Akahoji mpaka wa madaraka kati ya Serikali za Mitaa na Serikali Kuu unaanzia na kuishia wapi kiutendaji?

Mwanri alisema mkuu wa mkoa kwa mujibu wa Sheria ya Tawala za Mikoa Na.19 ya mwaka 1997, katika vifungu Na 5, 6 na 7 ana wajibu wa kusimamia kazi na shughuli zote za Serikali katika mkoa ikiwa  ni pamoja na kuziwezesha mamlaka za Serikali za Mitaa, kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu zilizotungwa na Bunge.

Alisema majukumu ya wakuu wa wilaya yametengwa katika kifungu Na.14 (1-3) cha Sheria ya Tamisemi, Na.19 ya mwaka 1997 kwamba yeye ndiye msimamizi mkuu wa shughuli za Serikali katika wilaya yake.

“Hivyo madaraka ya jumla ya mkuu wa wilaya yanatiririshwa kutoka kwa Mheshimiwa Rais kupitia kwa mkuu wa mkoa, kwa upande wa watendaji walio chini ya mkurugenzi wa halmashauri, wao ni watekelezaji wa shughuli za Serikali kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu zilizopo,” alisema.

Hata hivyo, alisema mipaka ya madaraka kati ya Serikali za Mitaa na Serikali Kuu imeanishwa katika Sheria za Mamlaka za Serikali za Mitaa na Sheria ya Tawala za Mikoa Na 19 ya 1997.

“Kwa kuzingatia sheria hizo ni kwamba mkuu wa mkoa na wilaya anaruhusiwa kuingilia kati inapotokea mamlaka za Serikali za Mitaa zimeshindwa kutekeleza majukumu yao au kukiuka misingi ya sera na sheria zilizopo.

Wednesday, January 11, 2012

Salam kutoka Finland

Elisha Magolanga in Turku Finland

The student tutor Klaudia Kakera with Elisha near student village in Turku

Michael Aboagye and Elisha soon after arrival at the Helsinki airport

An exchange programme student from Ghana, Michael Aboagye

Student tutor Maria with exchange programme students at Turku

The student tutor Maria (center) with Mkicahel, left and Elisha/ right outside the supermarket at Turku city

Tuesday, October 25, 2011

Mbunge aswekwa rumande kwa kuvamia kituo cha polisi

Mbunge wa Nzega Dk. Hamis Kigwangala

Na Moses Mabula, Nzega

MBUNGE wa Nzega, Dkt. Hamisi Kigwangala (CCM) amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Wilaya ya Nzega akikabiliwa
na makosa sita yakiwemo kuvamia kituo cha polisi wilayani hapa.

Dkt. Kigwangalla alitiwa mbaroni juzi na Jeshi la Polisi wilayani hapa huku akiwa na baadhi ya wananchi wa jimbo hilo, Bw. Mrisho Hamisi, Bw. Methew Dotto, Bw. Mwanja mwandu wote wakazi wa Kata ya Nata ambao ni badhi ya wachimbaji wadogowadogo waliokuwa katika vurugu zilizotokea juzi katika Kijiji cha Mwabangu.
 
Wakisomewa mashtaka na Waendesha Mashtaka Merito Ukingoji na Joseph Mbwana, ilidiwa kuwa walifanya mkusanyiko usio halali Oktoba 23 mwaka huu katika mgodi mdogo uliopo kijiji hicho.
 
Kosa la pili na la tatu ni kuingia katika mgodi mdogo unaomilikiwa na wawekezaji bila idhini ya wamiliki na kuvamia Kituo cha Polisi cha Nzega saa mmoja jioni.

Shitaka la nne kwa mujibu wa waendesha mashitaka hao ni kufanya njama katika ofisi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilaya na kufanya maandamano kuvamia Kituo cha Polisi.

Makosa mengine ni kupiga na kujeruhi watu waliotajwa kuwa ni Mosesi
kichambi na Feldinald Yusuph ambao wamejeruhi katika ghasia zilizotokea juzi baada ya wachimbaji wadogo kuchoka kunyanyaswa na kunyang'wanywa eneo lao.

Waendesha mashtaka hao walidai kuwa upelelezi wa tuhuma hizo bado unaendelea kubaini chanzo cha vurugu huku mbunge huyo akiwekewa pingamizi ya kutofika eneo hilo la mgodi kwa kile kilichodaiwa kuwa ni kuepusha tafrani inayoweza kujitokeza kwa wananchi na wawekezaji.
 
Mbele ya Hakimu Mkazi Wilaya ya Nzega, Ajali Milanzi, watuhumiwa hao walikana mashtaka hayo yote huku mbunge huyo akipewa dhamana baada ya kujidhamini mwenyewe kupitia nafasi yake, kisha kuwadhamini wenzake watatu.

hata hivyo Mahakama hiyo ilimpa dhamana hiyo kwa muda na kumwamuru kuwafikisha mahakamani hapo leo watuhumiwa wenzake aliowadhamini wakiwa na watu watakaowadhamini upya, vinginevyo mahakama hiyo itafuta dhamana kwa watu wote. Kesi hiyo imepangwa kusikilizwa Novemba 18, mwaka huu.

Mbunge azungumza
 
Baada ya kuachiwa, mbunge huyo alisema kitendo hicho cha kumweka ndani kimemdhalilisha vya kutosha hasa akiwa katika kudai haki ya wananchi wake ambao wamekuwa wakionewa mara kwa mara na wawekezaji hao.
 
"Nimeshangazwa na Jeshi la Polisi hasa OCD (Mkuu wa Polisi Wilaya) kunibambikia makosa ambayo hayana ukweli pamoja na kunidhalilisha kunipiga vibao kama mtoto mdogo na dhihaka mbalimbali kwa wananchi wangu ambao walikuwa wakidai haki yao ya msingi, hii si haki sikutendewa haki katika hili ni uonevu mtupu," alisema Dkt. Kigwangalla.
 
Aliapa kutokata tamaa kutetea haki na maslahi ya wananchi wake licha ya kugeuziwa kibao wakati gari lake lenye namba T 357 BMP aina ya Caldin lilipigwa mawe na kusababisha kuvunjika kioo cha mbele na kupigwa mawe yeye na wananchi wake wakidai haki.
1