Monday, October 17, 2011

Magamba yazidi kuitafuna CCM

Katibu wa itikadi na uenezi CCM Nape Nnauye akihutubia wanachi wa Mwanza


Mwanza

 FALSAFA ya kuvuana magamba nchini ya Chama Cha mapinduzi (CCM) imezidi kukitesa
chama hicho na kuzua mvutano baina ya viongozi na baadhi ya wanachama sasa ikielezwa kuwa lazima mageuzi hayo yaendelee vinginevyo hali itakuwa mbaya na nchi itashindwa kutawalika.

Wakati kumekuwapo na msuguano na maelezo kuwa Katibu wa Halmashauri Kuu, Itikadi na Uenezi, Bw. Nape Nnauye anapotosha maagizo ya chama chake kuhusu dhana hiyo, yeye ameibuka na kusema mageuzi yanayoendelea ndani ya chama hicho maarufu kama kujivua gamba ni ya kweli, na yakifanyika ipasavyo ni ukombozi kwa wananchi wanyonge wa Tanzania lakini machungu kwa kundi linalofaidika na jasho lao.

Akihutubia mamia ya wananchi katika mkutano wa hadhara jijini Mwanza jana kwenye viwanja vya Magomeni, Kirumba, Bw. Nnauye alisema mageuzi hayo ni ukombozi kwa wanyonge kwa kuwa yamelenga kuimarisha misingi ya uadilifu na kuwajibika kwa viongozi waliopewa dhamana.

"Ni rahisi leo kumkuta kiongozi anamiliki utajiri wa kutisha na kufuru kuliko hata kipato chake halali, tukisema tukae kimya nchi hii haitatawalika. Dawa ni kufanya mageuzi haya leo kabla hali haijachafuka sana," alisema na kuongeza.

Kwa mujibu wa Bw. Nnauye, kufanikiwa kwa mageuzi hayo kutasaidia kuhakikisha kunakuwapo mgawanyo mzuri wa rasilimali za nchi, hivyo kulewa ukombozi wa moja kwa moja kwa wanyonge nchini.

"Tusisahau ndugu zangu, nguvu ya chama hiki na heshima yake imekuwa ni kutetea wanyonge nchini, Afrika na duniani kwa ujumla. Kutetea wanyonge lazima uhakikishe rasilimali za nchi zinanufaisha wanyonge, bila uadilifu na kuwajibika haitawezekana, ndio malengo ya mageuzi tuyafanyayo," alisema Bw. Nnauye.

Alisisitiza kuwa misingi ya CCM na imani yake vikifuatwa na kusimamiwa vizuri kwa dhati bila unafiki kelele zinazosikika leo za matumizi mabaya ya rasilimali za nchi hazitakuwepo na kuweka wazi kuwa kundi linalofaidika na hali ya sasa, ndilo linalopotosha maana ya mageuzi hayo kwa kutoa hoja alizoita dhaifu.

Alisema kumejengeka utamaduni na hasa kwa baadhi ya watu wenye dhamana kujijali wao wenyewe zaidi kuliko wananchi wanaowaongoza, tabia ambayo imeongeza tofauti ya kipato kati ya wananchi wa chini na viongozi wao, huku wengine wakiwa na kipato kisichokuwa na maelezo sahihi.

"Mwalimu (Nyerere) aliwahi kuwahoji viongozi waliotaka uongozi wa juu wakati huo, kwa umri wenu na kipato chenu mmetoa wapi utajiri huu? Na hiyo ilitosha kumzuia mtu asigombee uongozi, leo ukihoji uadilifu wa baadhi ya viongozi utaandamwa wewe, usipokuwa makini wanakutoa roho," alisisitiza Bw. Nnauye.

Akitoa ufafanuzi zaidi Bw. Nnauye alionya kuwa kama tofauti ya kipato isiposhughulikiwa mapema na hasa kuwadhibiti wale wanaojilimbikizia mali kwa njia haramu wakiwemo viongozi na kugeuza chama kichaka chao, nchi itavurugika kwa kuwa wanyonge ni wengi na watatumia nguvu kudhibiti rasilimali zao na kudai usawa.
0

Monday, October 10, 2011

Mbunge wa NCCR ainyemelea CHADEMA



Mhe, Felix Mkosamali mbunge wa Muhambwe (Kigoma)
ndiye mbunge mdogo kuliko wote bungeni

Na Mwandishi wetu
Kuna kila dalili ya kufanyika kwa uchaguzi mwingine mdogo kwa upande wa Tanzania Bara, baada ya mbunge wa NCCR-Mageuzi Jimbo la Mhambwe, Felix Mkosamali kuanza mazungumzo na Chadema kwa lengo la kutaka kuhama chake cha sasa.
Tayari taifa lilishuhudia uchaguzi mdogo wa Igunga uliofanyika Oktoba mbili kujaza nafasi ya Rostam Aziz aliyejiuzu nyadhifa zote ndani ya CCM ikiwamo na ubunge kwa madai kuwa chama chake kinaendesha siasa za uchwara.
Wakati uchaguzi huo wa Igunga ukitajwa kutumia rasilimali nyingi za vyama vya siasa ikiwamo mabilioni ya fedha, Mkosamali ambaye ni mbunge kijana wa NCCR-Mageuzi anatajwa kufanya mazungumzo na Chadema na huenda akatangaza kujiuzulu wadhifa huo na unachama wa chama chake cha sasa wakati wowote.
                                                                                                                                        
Kwa mujibu wa washirika wa karibu wa Mkosamali, uamuzi huo unatokana na kile kinachoelezwa ni msuguano wake wa chini kwa chini na mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, James Mbatia.

Washirika hao wa karibu wa Mkosamali, walifafanua kwamba msuguano huo umemfanya mbunge huyo kufikiria uamuzi huo wa kuhama chama chake na kujiunga Chadema ambako anaamini anaweza kutimiza malengo yake kisiasa.
Hata hivyo, alipoulizwa mwenyewe kwa njia ya simu, alijibu kwa kifupi, "Kaka una haraka gani? Si unisubiri kesho (leo) unipigie? Kesho nitakwambia kila kitu. Kwanza nani kakupa hizi taarifa,? Aliuliza Mkosamali

Naye rafiki yake wa karibu Metusela Mawazo aliiambia Mwananchi kwamba naye amesikia taarifa za Mkosamali kutaka kuhamia Chadema kutokana na hali inayoendelea ndani ya NCCR-Mageuzi.
“Kimsingi nimezipata taarifa za Mkosamali kuanza harakati za kuhamia Chadema, zimenistusha sana. Ni taarifa za kweli na kama unavyojua mwananchi yoyote anaweza kuhamia chama anachokitaka,” alisema Mawazo.
Alisema kwa jinsi anavyomjua Mkosamali kimsimamo hayuko tayari kufanya kazi akiwa NCCR-Mageuzi. “Ni rafiki yangu wa karibu sana, hayuko tayari kufanya kazi akiwa NCCR-Mageuzi, ni mpambanaji na nina uhakika atashinda uchaguzi mdogo,” alisema Mawazo ambaye aligombea ubunge kwa tiketi ya NCCR-Mageuzi Jimbo la Buyungu Kibondo na kuchuana vikali na mgombea wa CCM, Christopher Chiza.

Mbatia akana msuguano

Hata hivyo, Mbatia alipoulizwa kuhusu hilo, alistuka huku akisema, ''Mimi sina msuguano na Mkosamali kwani hata juzi tulikuwa naye kwenye kikao. Tulifanya nae kikao na tukazungumza vizuri tu, hilo la msuguano ndiyo nasilikia kwako".

Mbatia alisema mwisho jana, aliwasiliana na Mkosamali ambaye alimtumia ujumbe mfupi wa simu akimwomba mwenyekiti huyo afuatilie vema kuhusu kesi yake ya jimbo la Mhambwe na kutaka chama kilijadili vema.

"Sasa nashangaa unavyoniambia anataka kuhama au nina msuguano nae. Leo (jana) alinitumia ujumbe mfupi kuhusu kesi ya uchaguzi jimbo lake la Mhambwe. Alitaka chama kijadili vema hilo na nikamwambia sawa," alisema Mbatia.

Hata hivyo, vyanzo zaidi vilivyo karibu na Mkosamali vilidokeza jana usiku kwamba Mbatia ameomba kukutana na mbunge huyo leo kwa ajili ya kujadili zaidi suala hilo ambalo linaweza kuwa pigo kuu kisiasa kwa NCCR-Mageuzi.
NCCR-Mageuzi katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka jana kilipata viti vinne vya majimbo ambavyo ni Kigoma Kusini kwa David Kafulila, Mhambwe kwa Mkosamali, Kasulu Vijini Zaitun Buyogela na Kasulu Mjini kwa Moses Machali.


CHANZO MWANANCHI

Telecommunication Workers Union of Tanzania in hot conflict again

By Elisha Magolanga TUICo
Telecommunication Workers Union of Tanzania (TEWUTA) leaders of Dar es Salaam branches have condemned the government and TTCL management to cooperate with non registered workers union in organizing workers interest. 
Addressing journalists in Dares Salaam yesterday, the Chairperson of TEWUTA Dar es Salaam Deogratias Machibya said that the Secretary General Junus Ndalo has betrayed the union by using TEWUTA umbrella to introduce Telecommunication Service Workers Union of Tanzania.
He said that TEWUTA is an illegal workers union that registered on 24th November 2004 under the Registrar of Trade Union (RTU) with Reg. no 018 which its members are TTCL workers only. 
“There is another union workers apart from TEWUTA emerged and took over TEWUTA mandate and authority to use members fund to enrich themselves. They have a marriage with TTCL management and government as a result of violation of workers rights” said Machibya.
Moreover, Machibya added that TEWUTA Dar es Salaam workers wrote a form TUF number 6 that directing Employer to install 2 percent union fee into their branches account but it has ignored and still install into unregistered workers union.
“Surprisingly the TTCL management has called the conversation meeting on 11th - 13th this month at Giraffe Ocean View Hotel to legitimate the contract no 162/2010 signed against the rule by that leaders” said Machibya.
He further added that all agenda to be discussed in the coming meeting it is against 67 (2) article of Employment and Labor Act no.6 of 2004 and its article no. 42 of 16th February 2007
Supporting to Machibya argument, the secretary General of TEWUTA Central Dar ea Salaam branch L. Ishengoma said they have committed to represent their fellow workers allover the country as they send them.
Ishengoma condemned Ndalo to break central council and executive council before election and refused to call for election according to TEWUTA constitution.
On the other side, the Secretary General of Telecommunication Workers Union of Tanzania Junus Ndalo said that it is not true that TEWUTA has changed and there is no new union introduced through TEWUTA umbrella.   
He said “In 17th December 2010 the TEWUTA central committee agreed to expand the union apart from having only TTCL workers according to the constitution hence now include union members from Air Aviation, Telesecurity, Posta, Tigo, Zantel, Vodacom, and Airtel”
Ndalo added that the complainant is just a small group of leaders that failed on 15th and 16th June 2011 election hence they create grievance to the new leadership that elected legally.  
Moreover, Ndalo said Shadrack Mbwilo and 8 his fellow complainant have already opened case number 15 of 2011 to the Labor Court and advised to wait for the court decisions.  

Sunday, October 9, 2011

Hali ya Dr. Mwakyembe yaleta utata

Naibu Waziri wa Ujenzi Dr. Harrison Mwakyembe
Na Mwandishi wetu

Naibu Waziri wa Ujenzi, Dk Harrison Mwakyembe, amekuwa na hali tete kiafya baada ya kuugua ugonjwa uliomsababisha kuvimba mwili wote.

Habari zilizopatikana na kuthibitishwa na yeye mwenyewe zinaeleza kuwa, alianza kuwashwa ngozi miezi mitatu iliyopita kabla ya hali kubadilika siku za karibuni na hatimaye kuvimba sehemu kubwa ya mwili wake.

Mwakyembe alilieleza gazeti hili jana kuwa, baada ya  hali yake kubadilika alianza kupata matibabu katika hospitali mbalimbali jijini Dar es Salaam akiwa nyumbani kwake Kunduchi Beach.Akizungumza na gazeti hili kwa shida, Dk Mwakyembe alisema hajui chanzo cha ugonjwa huo wa ngozi, daktari wake ndiye anaweza kuelezea kwa usahihi.

“Ni kweli naumwa nipo nyumbani, hata sura yangu imebadilika. Sasa hivi namsubiri daktari wangu, nilisikia natakiwa kupelekwa India kwa matibabu, nasubiri kauli yake si mimi niamue,” alisema na kuongeza;

“Siwezi kusema nimelishwa sumu, ninachosema mimi nimevimba kweli mwili mzima naumwa kweli hapa nimelala na sijui umenipataje kwa simu kwa sababu huwa siiwashi muda huu una bahati kweli”alisema Mwakyembe.

Mke wa Dk Mwakyembe  Mkewe Linah Mwakyembe alipozungumza kwa njia ya simu na Mwananchi Jumapili, alisema kwa mujibu wa daktari wake, Dk mumewe  anasumbuliwa na ugonjwa wa ngozi unaojulikana kitaalamu kama Exfoliative Dermatitis.
 “Alianza kuugua muda mrefu kidogo, kama miezi mitatu iliyopita, hali hiyo ilikuwa inatokea na kupotea hadi sasa ambapo hali imekuwa mbaya zaidi,” alisema.

Alisema madaktari waliomfanyia uchunguzi kwa nyakati tofauti katika kipindi hicho walitoa majibu tofauti na kuongeza kuwa wapo waliosema hali hiyo ilisababishwa na kisukari na mwingine ambaye hakutaka kutaja jina lake, alisema kulikuwa na chembechembe za sumu katika damu yake.

“Baada ya ngozi yake kubadilika sana na hali kuwa mbaya, tulienda hospitali na madaktari walitupa majibu tofauti, wapo waliosema ni kisukari na kuna mwingine alisema kuna chembechembe za sumu,” alisema Linah na kufafanua  kuwa daktari aliyedai hivyo hakuwapa maelezo zaidi.
Kwa mujibu wa Linah, ngozi ya Dk Mwakyembe inawasha na inakuwa kama inatoa mba mwili mzima hadi kichwani.

Aliongeza kuwa daktari wake ameshauri ufanyike uchunguzi wa kina zaidi ili kujua kama atahitajika kupatiwa matibabu nje ya nchi.

Friday, October 7, 2011

Mvuto wa Chadema waongeza idadi ya wapiga kura Igunga

Mwenyekiti wa CHADEMA mkoa wa tabora Mohamed Kansa
Na Elisha Magolanga

Kama zilivyo za ndoto za usiku zinapofikia kikomo baada ya pambazuko la alfajiri, ndivyo ilivyo hali ya Igunga sasa. Kwa kawaida hakuna anayependa ndoto tamu ikatizwe, lakini kama ndoto hiyo ni ya kutisha basi muotaji hupata ahuweni pale anapozinduka usingizini na kutambua kumbe ilikuwa ni ndoto.

Ni baada ya kumalizika uchaguzi mdogo kufuatia kujiuzulu kwa Rostam Aziz aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo kwa takribani miaka 17 baada ya kulitwaa mwaka 1994 kufuatia kifo cha Charles Kabeho aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo.

Imebakia historia kwa watu wa jimbo Igunga kwani wapo wanaotamani iwapo hekeka za kampeni zingeendelea. Hawa ni pamoja na wafanyabiashara ya nyumba za kulala wageni, mama ntilie, hoteli, vituo vya mafuta, baa, madereva wa taksii na maduka ya kila aina.

Kuna wale waliotamani kuona helikopita za CCM, CUF na CHADEMA zikiendelea kuteka anga la jimbo lao, lakini pia katika vijiwe vya kahawa vilijaza wateja kwa sababu ya gumzo la uchaguzi.

Wapo waliotamani kuendelea kuwaona na kuwasikiliza Dk. Wilbroad Slaa na Freeman Mbowe wa CHADEMA wakijenga hoja za kisiasa jukwaani huku wakipambwa na nyimbo za kuvutia kama ‘People’s Power’

Pia wapo waliopenda kumsikiliza Rais mstaafu Ndugu, Benjamini Mkapa na Ismail Aden Rage na bastora yake kiunoni wakimwaga sera za Chama Cha Mapinduzi kwa ufasaha zaidi huku wakivutiwa na jukwaa la bendi ya TOT na wasanii maarufu kama Ze Orijino Komedi.

Lakini pia wapo wale waliovutiwa sana kusikiliza hotuba ya Ismail Jusa na Julius Matatilo wakimnadi Mgombea wa CUF kwa umakini wa hali ya juu.

Kwa upande wa vyama vya siasa ni furaha kwa CCM waliobahatika kushinda huku huzuni na majonzi yakiviendea vyama vilivyoshindwa katika uchaguzi huu.

Binafsi napenda kuvipongeza vyama vyote vilivyoshiriki katika uchaguzi huo kwani wametumia haki yao ya kikatiba kuimarisha kidemokrasia nchini.

Katika uchaguzi vyama vinane vilishiriki katika uchaguzi mdogo wa Igunga. Vyama hivyo ni CCM, CHADEMA, CUF, SAU, UPDP, AFP, CHAUSTA na DP.

Wahenga walipata kusema “Chovya chovya humaliza buyu la asali” na mimi leo hii nataka niyatumie maneno haya kama msingi wa makala yangu.

Ninataka kijikita sana katika kutoa tathini ya uchaguzi huku tayari jimbo hilo likiwa limekwisha kuchukuliwa na Chama Cha Mapinduzi ambapo Dk. Dalaly Kafumu ni mbunge mteule kwa mujibu wa katiba ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania.

Napenda kuzungumzia zaidi vyama vitatu vya CCM, CHADEMA na CUF kwani hivyo ndivyo vyama vilivyoonyesha ushindani mkali ambao haujawahi kutokea katika historia ya Tanzania.

Kwanza kabisa ninataka nipingane na hoja ya Katibu wa itikadi na uenezi wa CCM Nape Nnauye kupitia vyombo vya habari kwamba, vurugu za wafuasi wa CHADEMA zilisababisha watu kutokujitokeza kupiga kura.

Hoja yangu ni kwamba idadi ya wapiga kura katika jimbo la Igunga ni watu 171,019 na watu waliojitokeza kupiga kura katika uchaguzi huu ni watu 53,672 ambayo ni sawa na asilimia 33.3

Ukilinganisha na uchaguzi mkuu wa mwaka jana ni watu wapatao elfu 40 ndiyo walipiga kura ambayo ni sawa na 27 asilimia hivyo mwaka huu kuna ongezeko la takribani asilimia nane.

Kwa mantiki hiyo basi kumbe wapiga kura wameongezeka kwa kuvutiwa na kukiamini Chama cha Demokrasia na Maendeleo ukilinganisha na mwaka jana ambapo CHADEMA haikusimamisha mgombea katika uchaguzi mkuu wa 2010.

Dhana hiyo inajithihirisha kuwa Rostam Aziz hakuwa na mpinzani hivyo wananchi walipuuza kwa kuamini wapige kura wasipige atashinda tuu na hii ndiyo sababu ya wapiga kura kupungua katika uchaguzi wa mwaka jana.

Vilevile kwa mtazamo huo ninadiriki kuamini kwamba kushiriki kwa CHADEMA katika uchaguzi huu kumeongeza idadi ya wapiga kura baada ya kuona kuna mgombea mpya ambaye ni Ndugu Joseph Kashindye wa CHADEMA.

Kwa upande wa CCM sioni kama ni ushindi wa kujivuna kama Nape anavyodai kwamba mkakati wa kukisafisha chama umefanikiwa kwa kuungwa mkono na wananchi wa Igunga.

Tumeshuhudia CCM ikipokonywa na CHADEMA zaidi ya kura elfu 9 ambazo ni sawa na asilimia 22 hivyo si suala la kujivuna kwa ushindi huo ukilinganisha na ushindi wa mwaka jana wa kura elfu 35 sawa na asilimia 72.

Ni wakati wa CCM kukaa chini na kujitathmini upya ili kubaini nini chanzo cha kukosa mvuto kwa wananchi hata kuzidi kushuka siku hata siku, kama mwanzo wa makala yangu nilivyo nukuu maneno ya wahenga “Chovya chovya humaliza buyu la asali” hivyo basi buyu la asali ya CCM linazidi kuisha kwa chovya chovya ya wapinzani.

Kwa upande wa Chama Cha Wananchi (CUF) pia kinapaswa kujitathimini upya ili kubaini nini chanzo cha kufanya vibaya kwenye uchaguzi huu ukizingatia kilikuwa na mtaji wa kura elfu 11 za uchaguzi wa mwaka jana.

Ni wazi kwamba kura hizo si mwingine aliyewapokonya isippokuwa ni CHADEMA. Kama Mtatiro alivyoeleza vyombo vya habari kuwa kuitwa ‘CCM B’ kumekigharimu chama hicho hata kikaanguka kwa kishindo. serikali ya umoja wa kitaifa huko visiwani Zanzibar ndiyo hasa chanzo cha kupoteza kura Igunga.

Yawezekana kabisa CUF ikashindwa kuunguruma tanzania Bara katika uchaguzi ujao hasa ukilinganisha ni kipindi kifupi sana cha umoja huo na CCM.

Kwa CHADEMA pia wanapaswa kupongezwa kwa kazi waliyofanya ndani ya muda mfupi na kupata kura 23,260 ambayo ni sawa na asilimia 44.32. ni vyema sasa wakajitathimini pia ili kubaini ni kasoro gani zilizowanyima ushindi.

Matokeo hayo yamepokelewa na wasomi kwa hisia tofauti tofauti. Tumemsikia Mhadhili wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) Dk Benson Bana akisema “matokeo hayo yameonyesha jinsi CCM kinavyozidi kupotea machoni mwa Watanzania”

Dk Bana aliongeza kuwa CCM hakiwezi kutembea kifu mbele wakati wananchi waliomchagua mbunge wa chama hicho hawafiki hata asilimia 50 ya idadi ya waliojiandikisha kupiga kura.

Bana aliongeza kuwa umefika wakati wa CCM kujitazama upya kwa kuwa CHADEMA kinakuja kwa kasi na kimejidhihirisha katika uchaguzi huo nkwa kupata kura nyingi licha ya kuwa hakikuwa na mtandao mkubwa katika jimbo hilo.

“Chadema wameibuka vizuri na wanaendelea kukubalika ila CCM kinazidi kupoteza ushawishi na mvuto wao kwa wananchi” alisema Bana.

Natoa wito kwa wananchi wa Igunga kwamba suala la kupiga kura ni muhimu sana kwa ustawi wa maendeleo ya jimbo lao. Kuchagua kiongozi bora ndiyo msingi wa maisha bora ya wana Igunga.

Hivyo basi, idadi ya watu waliojitokeza (33.3 asilimia) bado ni ndogo japokuwa imeongezeka kidogo ukilinganisha na mwaka jana.

Nawaomba vijana na wazee, wake kwa waume jitokezeni kwa wingi kujiandikisha kupiga kura muda utakapofika ili kuleta mabadiliko ya kweli katika taifa hili. Ni sisi tukiamua tunaweza kuijenga nchi kupitia viongozi waadilifu.

Thursday, October 6, 2011

Moto wateketeza ofisi za Star Times

Na Elisha Magolanga

Uchaguzi Igunga waigawa tena CCM

Na Moses Mabula, Tabora

SIKU tatu baada ya CCM kushinda uchaguzi wa Jimbo la Igunga, Mwenyekiti wa Chama hicho
mkoani Tabora, Bw. Hassan Wakasuvi ametoa siri ya wana-CCM wenzake wanaodaiwa wafuasi wa aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo, Bw. Rostam Aziz na swaiba wake, Bw. Edward Lowassa kuwa walitaka chama hicho kishindwe ili 'waheshimiane'.

Bw. Wakasuvi alitoa maneno hayo makali yaliyoambatana na vijembe, wakati akihutubia wana-CCM waliojikeza katika sherehe za kujipongeza kwa ushindi katika uchaguzi mdogo wa Igunga uliofanyika Oktoba 2, mwaka huu.

Katika uchaguzi huo, Bw. Dalali Kafumu wa CCM alishinda kiti hicho cha ubunge na hivyo kuchukua nafasi iliyoachwa wazi na Bw. Aziz.

Bw. Rostam alijiuzulu nyazifa zake zote za uongozi ndani ya CCM ukiwemo ubunge na ujumbe wa NEC Julai 14, 2011 kwa kile alichoita 'kuchoshwa na siasa uchwara', chuki na
kufitiniana miongoni mwa viongozi na wanachama.

Lakini kinyume na matarajio ya wengi, Bw. Aziz aliibuka kwenye uzinduzi wa kampeni na kuwaomba wakazi wa Igunga kumchagua mgombea wa CCM.

Katika hotuba yake hiyo, Bw. Wakasuvi alitumia muda mwingi kurusha vijembe na tambo, akisema, licha ya kwamba kulikuwepo na upinzani mkali kutoka nje ya chama na hata ndani ya
chama chake, kazi aliyoifanya inastahili kupongezwa na kwamba ushindi huo bila yeye CCM ingeambulia patupu.

“Najua wapo hapa miongoni mwetu ambao walitaka CCM ishindwe, hao nawapa pole na waende kliniki wakazae, maana tumeshinda. Lakini pia wapo waliotamani tupate ushindi hao nawapongeza na waendelee kushangilia, tumeshinda,” alisema Bw. Wakasuvi

“Watu hao walikuwa wakisema ni bora jimbo la Igunga tushindwe ili eti tuheshimiane, sasa tumeshinda naomba tuheshimiane” alisema.

“Mimi ndio nilikuwa mkuu wa majeshi huko Igunga, hakuna wakubisha, mimi ndo nilikuwa komandoo na nilikuwa naongoza mashambulizi dhidi ya wapinzani wetu kutoka ndani ya
CCM na wale kutoka vyama vya upinzani,” alitamba Bw. Wakasuvi.

“Kama ushindi tumepata ila najua wapo mliochukia pia najua mpo nyie mliofurahi, endeleeni kufarahia ili hawa waliochukia ikiwezekana wajinyonge," alisema Mwenyekiti huyo.

Utetezi kwa Mbunge Rage

Mwenyekiti huyo alivigeukia vyombo vya habari kwa kuvishambulia kwamba vilikuwa vinapendelea upande mmoja wa upinzani kutangaza taarifa za kampeni jimboni Igunga huku akimtetea mbunge wa Tabora Mjini, Bw. Ismail Rage kupanda jukwaani na bastola.

Bw. Wakasuvi alisema kuwa haoni tatizo la mbunge wake kupanda jukwaani na silaha kwa madai kuwa hali iliyokuwa Igunga mbunge wake alikuwa sahihi, na kwamba waandishi wa habari ndio waliolikuza suala hilo baada ya kuliripoti kwenye magazeti, lakini ni jambo la kawaida.

“Mimi mbona nilikuwa nayo kiunoni lakini hamkiniandika, nadhani mna chuki zenu na Rage nyie wanahabari,” alisema.

Bw. Wakasuvi anayeaminika kutoka kundi la Bw. Samuel Sitta ilielezwa kuwa katika kikao cha Kamati ya Siasa mkoa wa Tabora kilichofanyika wilayani Igunga kabla ya kuanza
kwa mchakato wa kampeni za uchaguzi huo, alimtuhumu Bw. Rostam na baadhi ya wafuasi wake kwa kusema, “hata kama mliomo humu ndani ya kikao mmenuna, hiyo ni shauri yenu,
CCM itashinda tu, kauli iliyoungwa mkono na mbunge wa Tabora mjini Bw. Aden Rage

Alisema “Hata kama Rostam ana pesa, hawezi kuwa maarufu kama CCM, hapa tutashinda uchaguzi hata bila yeye kuwepo," alikaririwa na waliohudhuria kikao hicho.

Alisema kwamba CCM ingeshinda uchaguzi kwa gharama yoyote ile kwa kuwa kina dola, kauli ambayo iliwakera baadhi ya waliohudhuria kikao hicho, na kumtaka arekebishe kauli yake kwamba kilichokuwa kinahitajika kwa sasa ni kuunganisha nguvu badala ya ubinafsi.

Katika kikao hicho kilichohudhuriwa pia na aliyekuwa Mratibu wa Kampeni za CCM, Bw. Nchemba, ilielezwa kuwa zaidi ya sh. milioni 800 zinahitajika ili kupata ushindi katika uchaguzi huo.

Wengine waliohudhuria mkutano huo ni Makamu Mwenyekiti wa CCM (bara), Bw. Pius Msekwa, mbunge Viti Maalum Bi. Munde Tambwe ambaye pia ni mjumbe NEC na Bw. Rage.

Mpashaji wa habari hizo, alilieleza gazeti hili kuwa Bw. Wakasuvi aliwaeleza wajumbe wa kikao hicho kuwa Bw. Aziz ameshindwa kuwaletea maendeleo wakazi wa jimbo la Igunga tangu
achaguliwe kushika nafasi hiyo mwaka 1994 baada ya kifo cha aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo, marehemu Charles Kabeho.

Habari kutoka ndani ya chama hicho mkoani hapa zinabainisha kuwa Bw. Wakasuvi haelewani na baadhi ya viongozi wenzake ndani ya CCM mkoa na wilaya kutokana na kile kilichoelezwa ni miongoni mwa waasisi wa chama cha CCJ, yeye na Bw. Sitta.

Hata hivyo, alipoulizwa kuhusu madai hayo na maelezo yake mkutanoni, Bw. Wakasuvi alikanusha huku akiuliza, “wewe umezipata wapi habari hizi wakati kwenye mkutano haukuwemo