Sunday, October 9, 2011

Hali ya Dr. Mwakyembe yaleta utata

Naibu Waziri wa Ujenzi Dr. Harrison Mwakyembe
Na Mwandishi wetu

Naibu Waziri wa Ujenzi, Dk Harrison Mwakyembe, amekuwa na hali tete kiafya baada ya kuugua ugonjwa uliomsababisha kuvimba mwili wote.

Habari zilizopatikana na kuthibitishwa na yeye mwenyewe zinaeleza kuwa, alianza kuwashwa ngozi miezi mitatu iliyopita kabla ya hali kubadilika siku za karibuni na hatimaye kuvimba sehemu kubwa ya mwili wake.

Mwakyembe alilieleza gazeti hili jana kuwa, baada ya  hali yake kubadilika alianza kupata matibabu katika hospitali mbalimbali jijini Dar es Salaam akiwa nyumbani kwake Kunduchi Beach.Akizungumza na gazeti hili kwa shida, Dk Mwakyembe alisema hajui chanzo cha ugonjwa huo wa ngozi, daktari wake ndiye anaweza kuelezea kwa usahihi.

“Ni kweli naumwa nipo nyumbani, hata sura yangu imebadilika. Sasa hivi namsubiri daktari wangu, nilisikia natakiwa kupelekwa India kwa matibabu, nasubiri kauli yake si mimi niamue,” alisema na kuongeza;

“Siwezi kusema nimelishwa sumu, ninachosema mimi nimevimba kweli mwili mzima naumwa kweli hapa nimelala na sijui umenipataje kwa simu kwa sababu huwa siiwashi muda huu una bahati kweli”alisema Mwakyembe.

Mke wa Dk Mwakyembe  Mkewe Linah Mwakyembe alipozungumza kwa njia ya simu na Mwananchi Jumapili, alisema kwa mujibu wa daktari wake, Dk mumewe  anasumbuliwa na ugonjwa wa ngozi unaojulikana kitaalamu kama Exfoliative Dermatitis.
 “Alianza kuugua muda mrefu kidogo, kama miezi mitatu iliyopita, hali hiyo ilikuwa inatokea na kupotea hadi sasa ambapo hali imekuwa mbaya zaidi,” alisema.

Alisema madaktari waliomfanyia uchunguzi kwa nyakati tofauti katika kipindi hicho walitoa majibu tofauti na kuongeza kuwa wapo waliosema hali hiyo ilisababishwa na kisukari na mwingine ambaye hakutaka kutaja jina lake, alisema kulikuwa na chembechembe za sumu katika damu yake.

“Baada ya ngozi yake kubadilika sana na hali kuwa mbaya, tulienda hospitali na madaktari walitupa majibu tofauti, wapo waliosema ni kisukari na kuna mwingine alisema kuna chembechembe za sumu,” alisema Linah na kufafanua  kuwa daktari aliyedai hivyo hakuwapa maelezo zaidi.
Kwa mujibu wa Linah, ngozi ya Dk Mwakyembe inawasha na inakuwa kama inatoa mba mwili mzima hadi kichwani.

Aliongeza kuwa daktari wake ameshauri ufanyike uchunguzi wa kina zaidi ili kujua kama atahitajika kupatiwa matibabu nje ya nchi.

Friday, October 7, 2011

Mvuto wa Chadema waongeza idadi ya wapiga kura Igunga

Mwenyekiti wa CHADEMA mkoa wa tabora Mohamed Kansa
Na Elisha Magolanga

Kama zilivyo za ndoto za usiku zinapofikia kikomo baada ya pambazuko la alfajiri, ndivyo ilivyo hali ya Igunga sasa. Kwa kawaida hakuna anayependa ndoto tamu ikatizwe, lakini kama ndoto hiyo ni ya kutisha basi muotaji hupata ahuweni pale anapozinduka usingizini na kutambua kumbe ilikuwa ni ndoto.

Ni baada ya kumalizika uchaguzi mdogo kufuatia kujiuzulu kwa Rostam Aziz aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo kwa takribani miaka 17 baada ya kulitwaa mwaka 1994 kufuatia kifo cha Charles Kabeho aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo.

Imebakia historia kwa watu wa jimbo Igunga kwani wapo wanaotamani iwapo hekeka za kampeni zingeendelea. Hawa ni pamoja na wafanyabiashara ya nyumba za kulala wageni, mama ntilie, hoteli, vituo vya mafuta, baa, madereva wa taksii na maduka ya kila aina.

Kuna wale waliotamani kuona helikopita za CCM, CUF na CHADEMA zikiendelea kuteka anga la jimbo lao, lakini pia katika vijiwe vya kahawa vilijaza wateja kwa sababu ya gumzo la uchaguzi.

Wapo waliotamani kuendelea kuwaona na kuwasikiliza Dk. Wilbroad Slaa na Freeman Mbowe wa CHADEMA wakijenga hoja za kisiasa jukwaani huku wakipambwa na nyimbo za kuvutia kama ‘People’s Power’

Pia wapo waliopenda kumsikiliza Rais mstaafu Ndugu, Benjamini Mkapa na Ismail Aden Rage na bastora yake kiunoni wakimwaga sera za Chama Cha Mapinduzi kwa ufasaha zaidi huku wakivutiwa na jukwaa la bendi ya TOT na wasanii maarufu kama Ze Orijino Komedi.

Lakini pia wapo wale waliovutiwa sana kusikiliza hotuba ya Ismail Jusa na Julius Matatilo wakimnadi Mgombea wa CUF kwa umakini wa hali ya juu.

Kwa upande wa vyama vya siasa ni furaha kwa CCM waliobahatika kushinda huku huzuni na majonzi yakiviendea vyama vilivyoshindwa katika uchaguzi huu.

Binafsi napenda kuvipongeza vyama vyote vilivyoshiriki katika uchaguzi huo kwani wametumia haki yao ya kikatiba kuimarisha kidemokrasia nchini.

Katika uchaguzi vyama vinane vilishiriki katika uchaguzi mdogo wa Igunga. Vyama hivyo ni CCM, CHADEMA, CUF, SAU, UPDP, AFP, CHAUSTA na DP.

Wahenga walipata kusema “Chovya chovya humaliza buyu la asali” na mimi leo hii nataka niyatumie maneno haya kama msingi wa makala yangu.

Ninataka kijikita sana katika kutoa tathini ya uchaguzi huku tayari jimbo hilo likiwa limekwisha kuchukuliwa na Chama Cha Mapinduzi ambapo Dk. Dalaly Kafumu ni mbunge mteule kwa mujibu wa katiba ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania.

Napenda kuzungumzia zaidi vyama vitatu vya CCM, CHADEMA na CUF kwani hivyo ndivyo vyama vilivyoonyesha ushindani mkali ambao haujawahi kutokea katika historia ya Tanzania.

Kwanza kabisa ninataka nipingane na hoja ya Katibu wa itikadi na uenezi wa CCM Nape Nnauye kupitia vyombo vya habari kwamba, vurugu za wafuasi wa CHADEMA zilisababisha watu kutokujitokeza kupiga kura.

Hoja yangu ni kwamba idadi ya wapiga kura katika jimbo la Igunga ni watu 171,019 na watu waliojitokeza kupiga kura katika uchaguzi huu ni watu 53,672 ambayo ni sawa na asilimia 33.3

Ukilinganisha na uchaguzi mkuu wa mwaka jana ni watu wapatao elfu 40 ndiyo walipiga kura ambayo ni sawa na 27 asilimia hivyo mwaka huu kuna ongezeko la takribani asilimia nane.

Kwa mantiki hiyo basi kumbe wapiga kura wameongezeka kwa kuvutiwa na kukiamini Chama cha Demokrasia na Maendeleo ukilinganisha na mwaka jana ambapo CHADEMA haikusimamisha mgombea katika uchaguzi mkuu wa 2010.

Dhana hiyo inajithihirisha kuwa Rostam Aziz hakuwa na mpinzani hivyo wananchi walipuuza kwa kuamini wapige kura wasipige atashinda tuu na hii ndiyo sababu ya wapiga kura kupungua katika uchaguzi wa mwaka jana.

Vilevile kwa mtazamo huo ninadiriki kuamini kwamba kushiriki kwa CHADEMA katika uchaguzi huu kumeongeza idadi ya wapiga kura baada ya kuona kuna mgombea mpya ambaye ni Ndugu Joseph Kashindye wa CHADEMA.

Kwa upande wa CCM sioni kama ni ushindi wa kujivuna kama Nape anavyodai kwamba mkakati wa kukisafisha chama umefanikiwa kwa kuungwa mkono na wananchi wa Igunga.

Tumeshuhudia CCM ikipokonywa na CHADEMA zaidi ya kura elfu 9 ambazo ni sawa na asilimia 22 hivyo si suala la kujivuna kwa ushindi huo ukilinganisha na ushindi wa mwaka jana wa kura elfu 35 sawa na asilimia 72.

Ni wakati wa CCM kukaa chini na kujitathmini upya ili kubaini nini chanzo cha kukosa mvuto kwa wananchi hata kuzidi kushuka siku hata siku, kama mwanzo wa makala yangu nilivyo nukuu maneno ya wahenga “Chovya chovya humaliza buyu la asali” hivyo basi buyu la asali ya CCM linazidi kuisha kwa chovya chovya ya wapinzani.

Kwa upande wa Chama Cha Wananchi (CUF) pia kinapaswa kujitathimini upya ili kubaini nini chanzo cha kufanya vibaya kwenye uchaguzi huu ukizingatia kilikuwa na mtaji wa kura elfu 11 za uchaguzi wa mwaka jana.

Ni wazi kwamba kura hizo si mwingine aliyewapokonya isippokuwa ni CHADEMA. Kama Mtatiro alivyoeleza vyombo vya habari kuwa kuitwa ‘CCM B’ kumekigharimu chama hicho hata kikaanguka kwa kishindo. serikali ya umoja wa kitaifa huko visiwani Zanzibar ndiyo hasa chanzo cha kupoteza kura Igunga.

Yawezekana kabisa CUF ikashindwa kuunguruma tanzania Bara katika uchaguzi ujao hasa ukilinganisha ni kipindi kifupi sana cha umoja huo na CCM.

Kwa CHADEMA pia wanapaswa kupongezwa kwa kazi waliyofanya ndani ya muda mfupi na kupata kura 23,260 ambayo ni sawa na asilimia 44.32. ni vyema sasa wakajitathimini pia ili kubaini ni kasoro gani zilizowanyima ushindi.

Matokeo hayo yamepokelewa na wasomi kwa hisia tofauti tofauti. Tumemsikia Mhadhili wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) Dk Benson Bana akisema “matokeo hayo yameonyesha jinsi CCM kinavyozidi kupotea machoni mwa Watanzania”

Dk Bana aliongeza kuwa CCM hakiwezi kutembea kifu mbele wakati wananchi waliomchagua mbunge wa chama hicho hawafiki hata asilimia 50 ya idadi ya waliojiandikisha kupiga kura.

Bana aliongeza kuwa umefika wakati wa CCM kujitazama upya kwa kuwa CHADEMA kinakuja kwa kasi na kimejidhihirisha katika uchaguzi huo nkwa kupata kura nyingi licha ya kuwa hakikuwa na mtandao mkubwa katika jimbo hilo.

“Chadema wameibuka vizuri na wanaendelea kukubalika ila CCM kinazidi kupoteza ushawishi na mvuto wao kwa wananchi” alisema Bana.

Natoa wito kwa wananchi wa Igunga kwamba suala la kupiga kura ni muhimu sana kwa ustawi wa maendeleo ya jimbo lao. Kuchagua kiongozi bora ndiyo msingi wa maisha bora ya wana Igunga.

Hivyo basi, idadi ya watu waliojitokeza (33.3 asilimia) bado ni ndogo japokuwa imeongezeka kidogo ukilinganisha na mwaka jana.

Nawaomba vijana na wazee, wake kwa waume jitokezeni kwa wingi kujiandikisha kupiga kura muda utakapofika ili kuleta mabadiliko ya kweli katika taifa hili. Ni sisi tukiamua tunaweza kuijenga nchi kupitia viongozi waadilifu.

Thursday, October 6, 2011

Moto wateketeza ofisi za Star Times

Na Elisha Magolanga

Uchaguzi Igunga waigawa tena CCM

Na Moses Mabula, Tabora

SIKU tatu baada ya CCM kushinda uchaguzi wa Jimbo la Igunga, Mwenyekiti wa Chama hicho
mkoani Tabora, Bw. Hassan Wakasuvi ametoa siri ya wana-CCM wenzake wanaodaiwa wafuasi wa aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo, Bw. Rostam Aziz na swaiba wake, Bw. Edward Lowassa kuwa walitaka chama hicho kishindwe ili 'waheshimiane'.

Bw. Wakasuvi alitoa maneno hayo makali yaliyoambatana na vijembe, wakati akihutubia wana-CCM waliojikeza katika sherehe za kujipongeza kwa ushindi katika uchaguzi mdogo wa Igunga uliofanyika Oktoba 2, mwaka huu.

Katika uchaguzi huo, Bw. Dalali Kafumu wa CCM alishinda kiti hicho cha ubunge na hivyo kuchukua nafasi iliyoachwa wazi na Bw. Aziz.

Bw. Rostam alijiuzulu nyazifa zake zote za uongozi ndani ya CCM ukiwemo ubunge na ujumbe wa NEC Julai 14, 2011 kwa kile alichoita 'kuchoshwa na siasa uchwara', chuki na
kufitiniana miongoni mwa viongozi na wanachama.

Lakini kinyume na matarajio ya wengi, Bw. Aziz aliibuka kwenye uzinduzi wa kampeni na kuwaomba wakazi wa Igunga kumchagua mgombea wa CCM.

Katika hotuba yake hiyo, Bw. Wakasuvi alitumia muda mwingi kurusha vijembe na tambo, akisema, licha ya kwamba kulikuwepo na upinzani mkali kutoka nje ya chama na hata ndani ya
chama chake, kazi aliyoifanya inastahili kupongezwa na kwamba ushindi huo bila yeye CCM ingeambulia patupu.

“Najua wapo hapa miongoni mwetu ambao walitaka CCM ishindwe, hao nawapa pole na waende kliniki wakazae, maana tumeshinda. Lakini pia wapo waliotamani tupate ushindi hao nawapongeza na waendelee kushangilia, tumeshinda,” alisema Bw. Wakasuvi

“Watu hao walikuwa wakisema ni bora jimbo la Igunga tushindwe ili eti tuheshimiane, sasa tumeshinda naomba tuheshimiane” alisema.

“Mimi ndio nilikuwa mkuu wa majeshi huko Igunga, hakuna wakubisha, mimi ndo nilikuwa komandoo na nilikuwa naongoza mashambulizi dhidi ya wapinzani wetu kutoka ndani ya
CCM na wale kutoka vyama vya upinzani,” alitamba Bw. Wakasuvi.

“Kama ushindi tumepata ila najua wapo mliochukia pia najua mpo nyie mliofurahi, endeleeni kufarahia ili hawa waliochukia ikiwezekana wajinyonge," alisema Mwenyekiti huyo.

Utetezi kwa Mbunge Rage

Mwenyekiti huyo alivigeukia vyombo vya habari kwa kuvishambulia kwamba vilikuwa vinapendelea upande mmoja wa upinzani kutangaza taarifa za kampeni jimboni Igunga huku akimtetea mbunge wa Tabora Mjini, Bw. Ismail Rage kupanda jukwaani na bastola.

Bw. Wakasuvi alisema kuwa haoni tatizo la mbunge wake kupanda jukwaani na silaha kwa madai kuwa hali iliyokuwa Igunga mbunge wake alikuwa sahihi, na kwamba waandishi wa habari ndio waliolikuza suala hilo baada ya kuliripoti kwenye magazeti, lakini ni jambo la kawaida.

“Mimi mbona nilikuwa nayo kiunoni lakini hamkiniandika, nadhani mna chuki zenu na Rage nyie wanahabari,” alisema.

Bw. Wakasuvi anayeaminika kutoka kundi la Bw. Samuel Sitta ilielezwa kuwa katika kikao cha Kamati ya Siasa mkoa wa Tabora kilichofanyika wilayani Igunga kabla ya kuanza
kwa mchakato wa kampeni za uchaguzi huo, alimtuhumu Bw. Rostam na baadhi ya wafuasi wake kwa kusema, “hata kama mliomo humu ndani ya kikao mmenuna, hiyo ni shauri yenu,
CCM itashinda tu, kauli iliyoungwa mkono na mbunge wa Tabora mjini Bw. Aden Rage

Alisema “Hata kama Rostam ana pesa, hawezi kuwa maarufu kama CCM, hapa tutashinda uchaguzi hata bila yeye kuwepo," alikaririwa na waliohudhuria kikao hicho.

Alisema kwamba CCM ingeshinda uchaguzi kwa gharama yoyote ile kwa kuwa kina dola, kauli ambayo iliwakera baadhi ya waliohudhuria kikao hicho, na kumtaka arekebishe kauli yake kwamba kilichokuwa kinahitajika kwa sasa ni kuunganisha nguvu badala ya ubinafsi.

Katika kikao hicho kilichohudhuriwa pia na aliyekuwa Mratibu wa Kampeni za CCM, Bw. Nchemba, ilielezwa kuwa zaidi ya sh. milioni 800 zinahitajika ili kupata ushindi katika uchaguzi huo.

Wengine waliohudhuria mkutano huo ni Makamu Mwenyekiti wa CCM (bara), Bw. Pius Msekwa, mbunge Viti Maalum Bi. Munde Tambwe ambaye pia ni mjumbe NEC na Bw. Rage.

Mpashaji wa habari hizo, alilieleza gazeti hili kuwa Bw. Wakasuvi aliwaeleza wajumbe wa kikao hicho kuwa Bw. Aziz ameshindwa kuwaletea maendeleo wakazi wa jimbo la Igunga tangu
achaguliwe kushika nafasi hiyo mwaka 1994 baada ya kifo cha aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo, marehemu Charles Kabeho.

Habari kutoka ndani ya chama hicho mkoani hapa zinabainisha kuwa Bw. Wakasuvi haelewani na baadhi ya viongozi wenzake ndani ya CCM mkoa na wilaya kutokana na kile kilichoelezwa ni miongoni mwa waasisi wa chama cha CCJ, yeye na Bw. Sitta.

Hata hivyo, alipoulizwa kuhusu madai hayo na maelezo yake mkutanoni, Bw. Wakasuvi alikanusha huku akiuliza, “wewe umezipata wapi habari hizi wakati kwenye mkutano haukuwemo

Tuesday, October 4, 2011

Dr. Nchimbi to launch exihibition in Butiama

The Minister for Information, Youth, Culture and Sports Dr. Emmanuel Nchimbi (MP) addressing journalists in Dar es Salaam today 

The Regional Commissioner of Mara, John Gabriel Tupa answering journalists questions in Dar es Salaam











Elisha Magolanga, Hussein Ndubikile TUICo

The Ministry of Information, Youth, Culture and Sports is expected to launch exhibition week of commemoration for 50 years of independence at Butiama village on 7th October this week.

Addressing to journalists in Dar es Salaam yesterday, the Minister for Information, Youth, Culture and Sports Dr. Emmanuel Nchimbi (MP) said that the exhibitions aimed to show different achievements reached by the ministry since 9th December 1961. 

“The exhibition will end up on 14th October parallel with launching of Uhuru torch races at Butiama village as commemoration to the death of Father of Nation, Mwl Julius Kambarage Nyerere who introduced Mwenge rally” said Nchimbi.

The Vice President of the United Republic of Tanzania, Dr. Mohamed Ghalib Bilal will be a guest of honor to launch the Uhuru torch rally as a part and parcel of 50 years commemoration of Tanzania mainland independence.

The exhibition week will comprise the ministry’s institution and others stakeholders sectors include media, youth, culture and sports.

Apart from exhibitions, the ministry has also prepared different sports competition like bao, soccer, netball, athletics, and bicycle riding.

The ministry will also show different documentaries and writings of national events from 1961 so that people will be aware of their country’s history.  

“We have planned the participation of youth volunteering on different social activities that will be performed in Butiama village” he said.

Meanwhile, the Regional Commissioner of Mara, John Gabriel Tupa said that nearly 90 percent of preparation has already completed, that include grounds for sports an exhibition.  

Answering the question concerning last year chaos happened during Mwenge races at Butiama, the Regional Commissioner said that the government has organized well security environment and ensured peace exhibition.      

Three arraigned with conspiracy and theft


By Hussein Ndubikile (TUICo)
Three Residents were arraigned in the Kinondoni Resident Magistrate court charged with conspiracy to commit an offence and stealing by servants.

The Police Prosecutor Syllvester Shilikale told Resident Magistrate Aniseta Nwangula that in the first count the accused Francis Kamisha(46),John Ciment(45),and Aderyada Desdery(26) both residents of Kinondoni commit an offence on uknown date and places within months of August and September this year,Kinondoni District together commit an offence namely stealing by servants.

In the second count both on or about the 9th September, this year at Reagent Estate Migombani Street area,Kinondoni District being employed by Synovate Co.Ltd they did steal various office documents worths 69,181,980/-the property of Synovate Co. Ltd.

The accused remanded after being failed to meet the bail condition

The case has adjourned until 5 0ctober this year for another mention.

Meanwhile, a resident of Kimara makaroni yesterday was appeared before Kinondoni Resident Magistrate court charged with rape.

The Police Prosecutor Rugenalila Kasalilo told Resident Magistrate Suzan Kihawa that the accused Nickson Raymond(17) commit offence on 26 August this year at King’ong’o,Kinondoni District.

The accused did carnal knowledge of fourteen (14) aged girls

The accused remanded until the further investigation completed.

The case has adjourned until 6 0ctober this year for another mention.

In another development, a twenty two aged man was arraigned before Kinondoni Resident Magistrate court charged with reckless driving a motor vehicle on the public road.

The Police Prosecutor Mohamed Kilongo said before Resident Magistrate Suzan Kihawa that  Noel Ndeki resident of Kawe Mzizini,Kinondoni District commit offence on 2 September this year at 00:01hrs a long Bagamoyo road of Mbuyuni area.

The accused was ridden a tri-cycle Reg No.T.856 ETG make Bajaj on the public road recklessly he failed to control while was riding on the road thus he did ride extremely as a result knocked motor vehicle Reg No.T.449 BKM make Toyota Land Cruiser which lead damage to motor vehicle and tri motor cycle.

The accused remanded after being failed to meet the bail condition.

The case has adjourned until 5 October this year for another mention.

On the other hand, a resident of Manzese, Kinondoni District appeared before Kinondoni Resident Magistrate court charged with armed robbery.

The Police Prosecutor Rugenalila Kasalilo told Resident Magistrate Batiseba John that the accused commit an offence on about 13 day of September this year at Afrika Sana,Kinondoni District.

The accused did steal Motor cycle make Toyo Model Key colour black with Reg No.T.648 BLJ valued at 1,500,000/- the property of Ramadhan Pongwa and immediately before stole used violence to obtain the said Motorcycle.

The accused remanded after being failed to meet the bail conditions.

The case has adjourned until 5 0ctober this year for another mention.