Tuesday, October 25, 2011

Mbunge aswekwa rumande kwa kuvamia kituo cha polisi

Mbunge wa Nzega Dk. Hamis Kigwangala

Na Moses Mabula, Nzega

MBUNGE wa Nzega, Dkt. Hamisi Kigwangala (CCM) amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Wilaya ya Nzega akikabiliwa
na makosa sita yakiwemo kuvamia kituo cha polisi wilayani hapa.

Dkt. Kigwangalla alitiwa mbaroni juzi na Jeshi la Polisi wilayani hapa huku akiwa na baadhi ya wananchi wa jimbo hilo, Bw. Mrisho Hamisi, Bw. Methew Dotto, Bw. Mwanja mwandu wote wakazi wa Kata ya Nata ambao ni badhi ya wachimbaji wadogowadogo waliokuwa katika vurugu zilizotokea juzi katika Kijiji cha Mwabangu.
 
Wakisomewa mashtaka na Waendesha Mashtaka Merito Ukingoji na Joseph Mbwana, ilidiwa kuwa walifanya mkusanyiko usio halali Oktoba 23 mwaka huu katika mgodi mdogo uliopo kijiji hicho.
 
Kosa la pili na la tatu ni kuingia katika mgodi mdogo unaomilikiwa na wawekezaji bila idhini ya wamiliki na kuvamia Kituo cha Polisi cha Nzega saa mmoja jioni.

Shitaka la nne kwa mujibu wa waendesha mashitaka hao ni kufanya njama katika ofisi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilaya na kufanya maandamano kuvamia Kituo cha Polisi.

Makosa mengine ni kupiga na kujeruhi watu waliotajwa kuwa ni Mosesi
kichambi na Feldinald Yusuph ambao wamejeruhi katika ghasia zilizotokea juzi baada ya wachimbaji wadogo kuchoka kunyanyaswa na kunyang'wanywa eneo lao.

Waendesha mashtaka hao walidai kuwa upelelezi wa tuhuma hizo bado unaendelea kubaini chanzo cha vurugu huku mbunge huyo akiwekewa pingamizi ya kutofika eneo hilo la mgodi kwa kile kilichodaiwa kuwa ni kuepusha tafrani inayoweza kujitokeza kwa wananchi na wawekezaji.
 
Mbele ya Hakimu Mkazi Wilaya ya Nzega, Ajali Milanzi, watuhumiwa hao walikana mashtaka hayo yote huku mbunge huyo akipewa dhamana baada ya kujidhamini mwenyewe kupitia nafasi yake, kisha kuwadhamini wenzake watatu.

hata hivyo Mahakama hiyo ilimpa dhamana hiyo kwa muda na kumwamuru kuwafikisha mahakamani hapo leo watuhumiwa wenzake aliowadhamini wakiwa na watu watakaowadhamini upya, vinginevyo mahakama hiyo itafuta dhamana kwa watu wote. Kesi hiyo imepangwa kusikilizwa Novemba 18, mwaka huu.

Mbunge azungumza
 
Baada ya kuachiwa, mbunge huyo alisema kitendo hicho cha kumweka ndani kimemdhalilisha vya kutosha hasa akiwa katika kudai haki ya wananchi wake ambao wamekuwa wakionewa mara kwa mara na wawekezaji hao.
 
"Nimeshangazwa na Jeshi la Polisi hasa OCD (Mkuu wa Polisi Wilaya) kunibambikia makosa ambayo hayana ukweli pamoja na kunidhalilisha kunipiga vibao kama mtoto mdogo na dhihaka mbalimbali kwa wananchi wangu ambao walikuwa wakidai haki yao ya msingi, hii si haki sikutendewa haki katika hili ni uonevu mtupu," alisema Dkt. Kigwangalla.
 
Aliapa kutokata tamaa kutetea haki na maslahi ya wananchi wake licha ya kugeuziwa kibao wakati gari lake lenye namba T 357 BMP aina ya Caldin lilipigwa mawe na kusababisha kuvunjika kioo cha mbele na kupigwa mawe yeye na wananchi wake wakidai haki.
1

TANGAZO LA MAHAFALI YA 14 CHUO KIKUU CHA TUMAINI IRINGA



Mkuu wa Chuo Kikuu cha Tumaini Iringa, Profesa. Nicholas Bangu anawaalika wahitimu wa mwaka 2011, familia, ndugu, jamaa, marafiki na umma kwa ujumla kwenye mahafali ya 14 ya chuo hicho yatakayofanyika siku ya Jumamosi ya tarehe 29 Oktoba mwaka huu. Mahafali yataanza saa 3:00 asubuhi chuoni hapo.

Mahafali yatatanguliwa na kongamano la wanataaluma (convocation) litakalofanyika siku ya Ijumaa ya tarehe 28 Oktoba, kuanzia saa 3:30 asubuhi chuoni hapo.

Wahitimu wote wanatakiwa kuthibitisha ushiriki wao na kuhudhuria mazoezi ya mahafali (rehearsal) bila kukosa. Wanafunzi wasiyohudhuria mazoezi hayo yatakayofanyika siku ya Ijumaa tarehe 28 Oktoba, saa 10:00 Jioni hawatashiriki kwenye mahafali.

Tafadhali thibitisha ushiriki wako kwa kutuma ujumbe (SMS) kwa simu namba 0767888596 ama barua pepe (email) pro@tumaini.ac.tz. Mwisho wa kuthibitisha ushiriki ni tarehe 23/10/2011.

Majoho ya mahafali yataanza kutolewa tarehe 24/10/2011. Mwisho wa kutoa mahojo ni tarehe 28 Oktoba 2011 saa 10:00 jioni. Majoho yatatolewa na ofisi za wakuu wa vitivo husika.

NYOTE MNAKARIBISHWA

Tuesday, October 18, 2011

PCCB urges religious leaders to corporate on corruption battle

Kinondoni regional Acting PCCB commander Frida Wikesi addresing religious leaders in Dar es Salaam 
By Elisha Magolanga TUICo, and Hussein Ndubikile TUICo
Religious leaders have been urged to use their position in the society and persuade their followers in the fight against corruption which is on the increase in recent years.
The call was made yesterday by Kinondoni regional Acting PCCB commander Frida Wikesi at a one day seminar on corruption for religious leaders in Dar es Salaam.
She said that due to the lust for quick richness among leaders from all walks of life, corruptions has become rampart in many places, something which can be easily defeated with joint efforts between the government and the religious leaders. 
The Acting commander explained since many people are now more educated on civic education than before, there is also increase and willingness in reportage of corruption acts.
“The fighting against corruption is the obligation of all citizens including religious leaders, it should not be the work of PCCB as some people think, your support is highly needed to make a difference” said Wikesi.
For his part, Full Gospel Bible Fellowship of Coast Diocese Bishop Mtemi Mathias said that some leaders lack fear of God hence involve in corruption acts which is a very set back to social justice, good governance and economic development.
 “It is impossible to end corruption actions if some section of the society including leaders will lack moral ethics which is key to integrity, honest, and dignity” He added.
The Bishop said that PCCB should educate people on the impacts of corruption from the grassroots level so that many people from the local level can get on board in the fight against the menace.
Rev. Wilbert Mwasumbi, who represented the Christian Council of Tanzania, cited poor social services like health, and education as the main sources of corruption through which the executives and leaders solicit bribe at the expense of poor people.
For his part, the Sheikh for Kinondoni District, Mohamed Muhenga said that Tanzanians should build a culture of hating corruption because it is a sin and causes injustice in the society.
He said all religious leaders must use their platforms to preach against corruption because it is against God’s willing.

He urged the ant-corruption body to make sure that it leaves no stone unturned in the war on corruption saying it denied poor people’s rights.
“The poor people are robbed of their rights, and their economy. There is a need to step up our efforts if the battle has to be won” he said.
Commenting on the participation of religion leaders in the battle, Imam for Ndugumbi Masjid, Ibrahim Kibwana said that religion leaders are the most trusted and influential people in the society which means their involvement can easily scale up the fight against corruption.


Monday, October 17, 2011

Magamba yazidi kuitafuna CCM

Katibu wa itikadi na uenezi CCM Nape Nnauye akihutubia wanachi wa Mwanza


Mwanza

 FALSAFA ya kuvuana magamba nchini ya Chama Cha mapinduzi (CCM) imezidi kukitesa
chama hicho na kuzua mvutano baina ya viongozi na baadhi ya wanachama sasa ikielezwa kuwa lazima mageuzi hayo yaendelee vinginevyo hali itakuwa mbaya na nchi itashindwa kutawalika.

Wakati kumekuwapo na msuguano na maelezo kuwa Katibu wa Halmashauri Kuu, Itikadi na Uenezi, Bw. Nape Nnauye anapotosha maagizo ya chama chake kuhusu dhana hiyo, yeye ameibuka na kusema mageuzi yanayoendelea ndani ya chama hicho maarufu kama kujivua gamba ni ya kweli, na yakifanyika ipasavyo ni ukombozi kwa wananchi wanyonge wa Tanzania lakini machungu kwa kundi linalofaidika na jasho lao.

Akihutubia mamia ya wananchi katika mkutano wa hadhara jijini Mwanza jana kwenye viwanja vya Magomeni, Kirumba, Bw. Nnauye alisema mageuzi hayo ni ukombozi kwa wanyonge kwa kuwa yamelenga kuimarisha misingi ya uadilifu na kuwajibika kwa viongozi waliopewa dhamana.

"Ni rahisi leo kumkuta kiongozi anamiliki utajiri wa kutisha na kufuru kuliko hata kipato chake halali, tukisema tukae kimya nchi hii haitatawalika. Dawa ni kufanya mageuzi haya leo kabla hali haijachafuka sana," alisema na kuongeza.

Kwa mujibu wa Bw. Nnauye, kufanikiwa kwa mageuzi hayo kutasaidia kuhakikisha kunakuwapo mgawanyo mzuri wa rasilimali za nchi, hivyo kulewa ukombozi wa moja kwa moja kwa wanyonge nchini.

"Tusisahau ndugu zangu, nguvu ya chama hiki na heshima yake imekuwa ni kutetea wanyonge nchini, Afrika na duniani kwa ujumla. Kutetea wanyonge lazima uhakikishe rasilimali za nchi zinanufaisha wanyonge, bila uadilifu na kuwajibika haitawezekana, ndio malengo ya mageuzi tuyafanyayo," alisema Bw. Nnauye.

Alisisitiza kuwa misingi ya CCM na imani yake vikifuatwa na kusimamiwa vizuri kwa dhati bila unafiki kelele zinazosikika leo za matumizi mabaya ya rasilimali za nchi hazitakuwepo na kuweka wazi kuwa kundi linalofaidika na hali ya sasa, ndilo linalopotosha maana ya mageuzi hayo kwa kutoa hoja alizoita dhaifu.

Alisema kumejengeka utamaduni na hasa kwa baadhi ya watu wenye dhamana kujijali wao wenyewe zaidi kuliko wananchi wanaowaongoza, tabia ambayo imeongeza tofauti ya kipato kati ya wananchi wa chini na viongozi wao, huku wengine wakiwa na kipato kisichokuwa na maelezo sahihi.

"Mwalimu (Nyerere) aliwahi kuwahoji viongozi waliotaka uongozi wa juu wakati huo, kwa umri wenu na kipato chenu mmetoa wapi utajiri huu? Na hiyo ilitosha kumzuia mtu asigombee uongozi, leo ukihoji uadilifu wa baadhi ya viongozi utaandamwa wewe, usipokuwa makini wanakutoa roho," alisisitiza Bw. Nnauye.

Akitoa ufafanuzi zaidi Bw. Nnauye alionya kuwa kama tofauti ya kipato isiposhughulikiwa mapema na hasa kuwadhibiti wale wanaojilimbikizia mali kwa njia haramu wakiwemo viongozi na kugeuza chama kichaka chao, nchi itavurugika kwa kuwa wanyonge ni wengi na watatumia nguvu kudhibiti rasilimali zao na kudai usawa.
0

Monday, October 10, 2011

Mbunge wa NCCR ainyemelea CHADEMA



Mhe, Felix Mkosamali mbunge wa Muhambwe (Kigoma)
ndiye mbunge mdogo kuliko wote bungeni

Na Mwandishi wetu
Kuna kila dalili ya kufanyika kwa uchaguzi mwingine mdogo kwa upande wa Tanzania Bara, baada ya mbunge wa NCCR-Mageuzi Jimbo la Mhambwe, Felix Mkosamali kuanza mazungumzo na Chadema kwa lengo la kutaka kuhama chake cha sasa.
Tayari taifa lilishuhudia uchaguzi mdogo wa Igunga uliofanyika Oktoba mbili kujaza nafasi ya Rostam Aziz aliyejiuzu nyadhifa zote ndani ya CCM ikiwamo na ubunge kwa madai kuwa chama chake kinaendesha siasa za uchwara.
Wakati uchaguzi huo wa Igunga ukitajwa kutumia rasilimali nyingi za vyama vya siasa ikiwamo mabilioni ya fedha, Mkosamali ambaye ni mbunge kijana wa NCCR-Mageuzi anatajwa kufanya mazungumzo na Chadema na huenda akatangaza kujiuzulu wadhifa huo na unachama wa chama chake cha sasa wakati wowote.
                                                                                                                                        
Kwa mujibu wa washirika wa karibu wa Mkosamali, uamuzi huo unatokana na kile kinachoelezwa ni msuguano wake wa chini kwa chini na mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, James Mbatia.

Washirika hao wa karibu wa Mkosamali, walifafanua kwamba msuguano huo umemfanya mbunge huyo kufikiria uamuzi huo wa kuhama chama chake na kujiunga Chadema ambako anaamini anaweza kutimiza malengo yake kisiasa.
Hata hivyo, alipoulizwa mwenyewe kwa njia ya simu, alijibu kwa kifupi, "Kaka una haraka gani? Si unisubiri kesho (leo) unipigie? Kesho nitakwambia kila kitu. Kwanza nani kakupa hizi taarifa,? Aliuliza Mkosamali

Naye rafiki yake wa karibu Metusela Mawazo aliiambia Mwananchi kwamba naye amesikia taarifa za Mkosamali kutaka kuhamia Chadema kutokana na hali inayoendelea ndani ya NCCR-Mageuzi.
“Kimsingi nimezipata taarifa za Mkosamali kuanza harakati za kuhamia Chadema, zimenistusha sana. Ni taarifa za kweli na kama unavyojua mwananchi yoyote anaweza kuhamia chama anachokitaka,” alisema Mawazo.
Alisema kwa jinsi anavyomjua Mkosamali kimsimamo hayuko tayari kufanya kazi akiwa NCCR-Mageuzi. “Ni rafiki yangu wa karibu sana, hayuko tayari kufanya kazi akiwa NCCR-Mageuzi, ni mpambanaji na nina uhakika atashinda uchaguzi mdogo,” alisema Mawazo ambaye aligombea ubunge kwa tiketi ya NCCR-Mageuzi Jimbo la Buyungu Kibondo na kuchuana vikali na mgombea wa CCM, Christopher Chiza.

Mbatia akana msuguano

Hata hivyo, Mbatia alipoulizwa kuhusu hilo, alistuka huku akisema, ''Mimi sina msuguano na Mkosamali kwani hata juzi tulikuwa naye kwenye kikao. Tulifanya nae kikao na tukazungumza vizuri tu, hilo la msuguano ndiyo nasilikia kwako".

Mbatia alisema mwisho jana, aliwasiliana na Mkosamali ambaye alimtumia ujumbe mfupi wa simu akimwomba mwenyekiti huyo afuatilie vema kuhusu kesi yake ya jimbo la Mhambwe na kutaka chama kilijadili vema.

"Sasa nashangaa unavyoniambia anataka kuhama au nina msuguano nae. Leo (jana) alinitumia ujumbe mfupi kuhusu kesi ya uchaguzi jimbo lake la Mhambwe. Alitaka chama kijadili vema hilo na nikamwambia sawa," alisema Mbatia.

Hata hivyo, vyanzo zaidi vilivyo karibu na Mkosamali vilidokeza jana usiku kwamba Mbatia ameomba kukutana na mbunge huyo leo kwa ajili ya kujadili zaidi suala hilo ambalo linaweza kuwa pigo kuu kisiasa kwa NCCR-Mageuzi.
NCCR-Mageuzi katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka jana kilipata viti vinne vya majimbo ambavyo ni Kigoma Kusini kwa David Kafulila, Mhambwe kwa Mkosamali, Kasulu Vijini Zaitun Buyogela na Kasulu Mjini kwa Moses Machali.


CHANZO MWANANCHI

Telecommunication Workers Union of Tanzania in hot conflict again

By Elisha Magolanga TUICo
Telecommunication Workers Union of Tanzania (TEWUTA) leaders of Dar es Salaam branches have condemned the government and TTCL management to cooperate with non registered workers union in organizing workers interest. 
Addressing journalists in Dares Salaam yesterday, the Chairperson of TEWUTA Dar es Salaam Deogratias Machibya said that the Secretary General Junus Ndalo has betrayed the union by using TEWUTA umbrella to introduce Telecommunication Service Workers Union of Tanzania.
He said that TEWUTA is an illegal workers union that registered on 24th November 2004 under the Registrar of Trade Union (RTU) with Reg. no 018 which its members are TTCL workers only. 
“There is another union workers apart from TEWUTA emerged and took over TEWUTA mandate and authority to use members fund to enrich themselves. They have a marriage with TTCL management and government as a result of violation of workers rights” said Machibya.
Moreover, Machibya added that TEWUTA Dar es Salaam workers wrote a form TUF number 6 that directing Employer to install 2 percent union fee into their branches account but it has ignored and still install into unregistered workers union.
“Surprisingly the TTCL management has called the conversation meeting on 11th - 13th this month at Giraffe Ocean View Hotel to legitimate the contract no 162/2010 signed against the rule by that leaders” said Machibya.
He further added that all agenda to be discussed in the coming meeting it is against 67 (2) article of Employment and Labor Act no.6 of 2004 and its article no. 42 of 16th February 2007
Supporting to Machibya argument, the secretary General of TEWUTA Central Dar ea Salaam branch L. Ishengoma said they have committed to represent their fellow workers allover the country as they send them.
Ishengoma condemned Ndalo to break central council and executive council before election and refused to call for election according to TEWUTA constitution.
On the other side, the Secretary General of Telecommunication Workers Union of Tanzania Junus Ndalo said that it is not true that TEWUTA has changed and there is no new union introduced through TEWUTA umbrella.   
He said “In 17th December 2010 the TEWUTA central committee agreed to expand the union apart from having only TTCL workers according to the constitution hence now include union members from Air Aviation, Telesecurity, Posta, Tigo, Zantel, Vodacom, and Airtel”
Ndalo added that the complainant is just a small group of leaders that failed on 15th and 16th June 2011 election hence they create grievance to the new leadership that elected legally.  
Moreover, Ndalo said Shadrack Mbwilo and 8 his fellow complainant have already opened case number 15 of 2011 to the Labor Court and advised to wait for the court decisions.